Quantcast
Channel: Fadhy Mtanga
Viewing all 76 articles
Browse latest View live

Haki ya wafanyakazi kugoma kwa mujibu wa sheria

$
0
0

MGOMO wa wafanyakazi ni ile hali ya wafanyakazi kusitisha ufanyaji kazi kwa muda fulani ili kumlazimisha mwajiri wao akubaliane na madai yao.  Ni njia ambayo wafanyakazi huitumia katika kumshinikiza mwajiri wao ayaridhie madai yao. 

Kifungu cha 4 cha Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini, Na. 6 ya mwaka 2004 kinatafsiri ‘mgomo’ kama kuacha kwa jumla au kiasi kufanya kazi na wafanyakazi kama kuacha huko ni kwa kumlazimisha mwajiri wao, au mwajiri yoyote mwingine, au chama cha waajiri ambacho mwajiri amejiunga, kukubali, kurekebisha au kuacha madai yoyote ambayo ni kiini cha mgogoro.

Kwa mantiki ya tafsiri hii ya sheria, mgomo ni zao la kushindikana kusuluhishwa kwa mgogoro baina ya wafanyakazi na mwajiri wao.  Mgogoro baina ya wafanyakazi na mwajiri wao huweza kusuluhishwa kwa njia ya majadiliano ya pamoja, usuluhishi, upatanishi, ama uamuzi.

Kama ilivyofafanuliwa na Kanuni ya 39(2) ya Kanuni za Ajira na Mahusiano kazini, mgomo wa wafanyakazi ni njia halali ya kuweka msukumo wa kiuchumi ili kusuluhisha migogoro ya maslahi kati ya waajiri na wafanyakazi.

Kwa hivyo basi, mgomo ni silaha ya mwisho kabisa ambayo wafanyakazi huitumia baada ya njia mbadala za kusuluhisha mgogoro baina yao na mwajiri wao kuwa zimeshindikana.  Inapoondokea njia hizi mbadala kuwa zimeshindikana, ndipo wafanyakazi wanapata haki ya kisheria ya kuitisha na kushiriki katika mgomo wao dhidi ya mwajiri wao.

Haki hiyo kwa wafanyakazi, wamepewa kwa mujibu ya kifungu cha 75(a) ya Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini, kwamba, “kila mfanyakazi ana haki ya kugoma kuhusiana na mgogoro wa maslahi”.

Mgogoro wa maslahi ni mgogoro wowote unaotokea mahali pa kazi ambao siyo lalamiko.  Kwa maana hiyo, mgogoro ambao hautokani na matumizi, tafsiri ama utekelezaji wa Makubaliano au mkataba wa ajira, mkataba wa hiari, Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini ama sheria yoyote nyingine iliyoandikwa inayosimamiwa na Waziri wa Kazi, utahesabika kuwa ni mgogoro wa maslahi.

Mgogoro wa maslahi umefafanuliwa pia kwa mujibu wa Kanuni ya 41(2) ya Kanuni za Ajira na Mahusiano Kazini (Kanuni za Utendaji Bora) za mwaka 2007 kuwa “ni mgogoro juu ya suala la kazi ambapo mwajiriwa hana haki kisheria na mwajiriwa anajaribu kuanzisha haki hiyo kwa kupata mwafaka kutoka kwa mwajiri”.

Tuchukulie mfano madai ya walimu, yaliyopelekea wao kutangaza mgomo.  Madai hayo ni, “ongezeko la mishahara kwa asilimia 100, posho ya kufundishia kwa walimu wa sayansi ya asilimia 55, asilimia 50 walimu wa masomo ya sanaa na asilimia 30 kwa walimu wanaofundisha katika mazingira magumu”. (Mwananchi, Julai 30, 2012)

Mgogoro huu wa maslahi unapaswa usuluhishwe kwanza kwa njia zilizowekwa kwa mujibu wa sheria.  Njia hizo zisipozaa matunda, wafanyakazi wanaweza kugoma. 

Kama walivyoeleza Rutinwa na wenzake (2011) haki ya wafanyakazi kugoma haipo ilimradi tu.  Inayo masharti yake.  Masharti hayo yaliyowekwa kwa mujibu wa Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini ndiyo yanayoufanya mgomo wa wafanyakazi kuwa halali ama la.

Masharti hayo yametajwa kwenye kifungu cha 80(1) aya ya (a) hadi (e) kwamba, wafanyakazi wanaweza kushiriki kwenye mgomo halali ikiwa:

(a) mgogoro ni mgogoro wa maslahi.  Kama nilivyoeleza awali, mgogoro wa maslahi unatokana na mambo ambayo si haki ya wafanyakazi kwa wakati huo, bali wanayapigania yawe haki yao.

(b) mgogoro umepelekwa kwa utaratibu uliowekwa kwenye Tume kwa usuluhishi.  Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini inataka mgogoro kupelekwa kwenye Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) ambayo imeanzishwa kwa mujibu wa kifungu cha 12 cha Sheria ya Taasisi za Kazi, Na. 7 ya mwaka 2004.  Utaratibu unautaka upande wenye madai kuyawasilisha kwenye Tume kwa kutumia utaratibu maalumu ili mgogoro huo ufanyiwe usuluhishi.

(c) mgogoro umebaki bila kutatuliwa hadi mwisho wa kipindi cha usuluhishi uliowekwa.  Maana yake ni kwamba, endapo muda uliowekwa kisheria kusuluhishwa kwa mgogoro huo utakwisha bila mgogoro huo kutatuliwa.  Muda huo kwa mujibu wa Kifungu cha 86(4) cha Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini ni siku 30, ama siku zingine zozote ambazo pande mbili za mgogoro zitakuwa zimekubaliana kwa maandishi.

(d) mgomo umeitishwa na chama cha wafanyakazi, kura zimepigwa chini ya katiba ya chama na wengi ya wale waliopiga kura wameunga mkono mgomo.  Kwa mantiki hii, mgomo ili uwe halali ni lazima uwe umeitishwa na chama cha wafanyakazi kilichosajiliwa kwa mujibu wa Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini. Si tu chama kisajiliwe, bali pia kinapaswa kutisha kura ili wanachama wake waamue.  Endapo kura nyingi zitaazimia kufanya mgomo, ndipo chama hicho kinapopata haki kisheria kuitisha mgomo huo, lakini kwa kufuata sharti linalofuatia.

(e) baada ya muda wa maombi uliotajwa katika aya ya (c), wao au chama chao wametoa taarifa ya saa arobaini na nane kwa mwajiri wao kuhusiana na nia yao ya kugoma.  Maana yake ni kwamba, baada ya masharti hayo hapo juu kuwa yametekelezwa, chama cha wafanyakazi kinapaswa kumpa mwajiri wao taarifa ya saa arobaini na nane ya kusudio lao la kugoma.

Masharti hayo yakifuatwa vema, ndipo wafanyakazi wanapopata haki ya kugoma.  Jambo la msingi la kuzingatia hapa, ni kuwa lazima mgogoro uwe ni mgogoro wa kimaslahi ambao umeshindikana kusuluhishwa chini ya Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA), uwe umeitishwa na chama cha wafanyakazi, na taarifa ya saa arobaini na nane iwe imetolewa. 

Hata hivyo, Sheria haimzuii msuluhishi kuendelea kusuluhisha mgogoro huo hata wakati wa mgomo.  Pia, Kanuni za Ajira na Mahusiano Kazini zinwataka wafanyakazi waliotangaza mgomo kuteua wawakilishi watakaokuwa na jukumu la kuhakikisha kanuni zinafuatwa, na kuhakikisha usalama wa himaya ya mwajiri unazingatiwa.

Kwa kuwa migomo huleta usitishwaji wa ufanyaji wa kazi, mwajiri hupata athari katika uzalishaji wa bidhaa na utoaji wa huduma kwa jamii.  Kama ambavyo tumekuwa tukishuhudia Tanzania namna ambavyo mgomo wa madaktari ulileta athari kubwa sana katika utoaji wa huduma ya afya, ama kama ambavyo mgomo wa sasa wa walimu unavyoleta athari katika utoaji wa elimu Tanzania.

Migomo ya wafanyakazi si jambo jema.  Lakini ni silaha muhimu mno pale ambapo njia za kawaida zinashindwa kutatua mgogoro wa maslahi baina ya wafanyakazi na mwajiri wao.  Wafanyakazi ambao ni wauzaji wa nguvu kazi yao, kama walivyo wauzaji wengine wa bidhaa, wanao uhuru wa kukataa kuuza nguvu kazi yao kwa bei isiyowanufaisha ama kwa masharti yasiyo rafiki kwao.


Siku Koero Mkundi alipochangamsha jamvi

$
0
0
Ilikuwa Septemba 7, 2010 miaka miwili nyuma.  Bofya hapa.
KOERO UTAOLEWA NA NANI? BADO NI KITENDAWILI, LAKINI LABDA MARKUS AU MTANGA…………….LOL

Najua wengi watashangaa maana wanajua mie sioleki, lakini naamini mmeona wenyewe jinsi wanaume hao wawili wanavyojifaragua, kwa mie binti kimwana.

Nakumbuka kuna mdau mmoja aliwahi kudai tena humu humu kwenye kibaraza cha Vukani kuwa mie sifai kuolewa na sitakuwa na ndoa imara kwa sababu eti nina kiherehere na kiroho papo cha kudai haki za wanawake.
Lakini Waswahili walishawahi kusema kuwa kama ni kibaya waachie wenzio……… sasa je kiko wapi?
Najua wahafidhina watatia fitina (hata hivyo nimeshawazoea) lakini wakae wakijua kuwa bahati imenidondokea….LOL
Ila kuna jambo moja, niliwahi kumuuliza bibi Koero kuhusiana na swala la wapiga emcheku kugongana kwa binti mmoja, Je inakuwaje? Jibu lilikuwa ni rahisi sana……. Ni kwamba watakaribishwa mmoja baada ya mwingine kupata mlo na baba mkwe na yule atakayekuwa anakata matonge makubwa ya ugali aka nguna na kula ugali mwingi unaofikia kilo moja kasorobo ndiye atakayepewa jiko,kwani hiyo ni ishara kuwa huyo atakuwa ni mkulima hodari na binti yao hatakufa na njaa.
Hivyo nawaomba wamezea mate na wasalandiaji waanze kuchukua mazoezi ya kumega matonge makubwa…. La sivyo hakuna ndoa….LOL
Na kwa maandalizi, wiki ijayo mwanamwali nawekwa ndani kusubiri hatima ya ndoa yangu……..je ni nani atapata bahati ya kujivinjari na kimwana……. Usikose kusoma hapa.

Na Koero Mkundi at 8:59 AM

Reactions:

33 comments:

Yasinta Ngonyani said...

Hapa kuna utamu hapa sijui itakuwaje maana nimeoona Markus na Mtanga wanaitana SHEMEJI na sasa wanamgombania mdogo wangu wa hiari aisee kaazi kweli kweli mie nasubiri kuona huyu atakaye weza nanunukuu:- "kula ugali mwingi unaofikia kilo moja kasorobo ndiye atakayepewa jiko,kwani hiyo ni ishara kuwa huyo atakuwa ni mkulima hodari na binti yao hatakufa na njaa."

September 17, 2010 10:50 AM

Fadhy Mtanga said...

Kwa vigezo hivyo vilivyoainishwa, namshauri shemeji yangu mtani Markus aanze kutafuta ustaarabu mwingine. Hii ngoma keshaikosa.

September 17, 2010 11:01 AM

Markus Mpangala said...

Kabla sijaandika katika KIJIJI changu cha KARIBUNI nyasanilifanya uchunguzi mara kadhaa, nimesoma mawasiliano yangu na huyu Koero, nikahitimisha 'ndiye nilikuwa nikimsaka miaka yote hii'. Asinidanganye mtu wala Mtani a.k.a SHEMEJI, Koero ni bonge la dhahabu SIPENDI wanawake wanaotazama vidume kama ndiyo mwisho wa maisha yao.
Koero napiga magoti NAOMBA TUOANE achana na mtani wangu Fadhy..... mie sina jingine sina cha kupindisha wala nini KOERO unatafutwa na mzee wa lundunyasa. sitanii kuna vitu nimegundua na nimeviona. ngoja nitaandika tena. HEBU FIKIRIA KWANINI NILIAMUA KUANDIKA HADHARANI DHAMIRA YANGU YA DHATI KUKUCHUMBIA na UWE MAMA WATOTO WANGU. nina hakika napigania nafasi yangu kwako. NAPIGA GOTI KWAKO binti Mkundi.
USISAHAU KUNISOMA PALE KIJIJI KWANGU karibuni nyasa.

September 17, 2010 11:33 AM

Anonymous said...

Ha ha ha haaaaaaa....Duh ugali kilo moja kasorobo....naamini akitokea msukuma itakuwa kaaazi kweli kweli, maan ataomba na nyongeza.......

September 17, 2010 11:45 AM

chib said...

Ha ha haaa, nimecheka.
Sipendi kuingilia chochote hapa, maana naona kama usiku wa kiza, kwani kuna wakati watu waliambiwa wameangukia pua kwa tamaa zao, sasa..... naona wameanikwa tena ha ha haaaa.
Kutokana na kusoma haraka haraka, basi yaonekana wote watatu mmepania, yaani Markus, Fadhy na Koero, na kuna wengine wameshawasha indicator na kuanza kutamba kabisaaaaaa, he he heeeee, nani alisema haolewi mtu.. ha ha haaa.
Ebu yamalizeni wenyewe nyuma ya pazia, sie tutakuja kuwaunga mkono kwa hali na mali katika kufanikisha muungano huo, ambao mpaka sasa bado ni wa kufikirika, ha ha haaaa

September 17, 2010 12:18 PM

John Mwaipopo said...

hadi raha vile. koero una visa wewe

September 17, 2010 12:33 PM

Anonymous said...

Halo haloooooo..... kule Tanga wanasema "mamie mwali tandika kwani mgeni anaingia" nami nasema Mama Koero jiandae Koero amepata jiko.......LOL

September 17, 2010 2:30 PM

Anonymous said...

Halo haloooooo..... kule Tanga wanasema "mamie mwali tandika kwani mgeni anaingia" nami nasema Mama Koero jiandae Koero amepata jiko.......LOL

September 17, 2010 2:30 PM

SIMON KITURURU said...

Mmmmh!

September 17, 2010 3:48 PM

Bwaya said...

Nimecheka. Matonge makubwa? Uhusiano wa matonge makubwa na kazi wapi wapi?
Lakini Koero, kama mwanaume mmoja anaweza kuoa wanawake zaidi ya mmoja; na kwa kuwa Koero wewe ni mtetezi wa usawa na haki za wanawake; huoni kwamba unaweza kabisa kuolewa na wote wawili ili kupunguza usumbufu wa hao jamaa kushindana kukata matonge?

September 17, 2010 3:52 PM

Fadhy Mtanga said...

This comment has been removed by the author.
September 17, 2010 4:53 PM

Fadhy Mtanga said...

naona shemeji yangu mtani Markus unajieleeeeza weee utadhani tupo kwenye jukwaa la ubunge.
mie siyo fundi wa maneno, bali vitendo.
natoa ushauri kwako shemeji uanze tu kucheki ustaarabu mwingine, hii ngoma ushaikosa.

September 17, 2010 5:00 PM

Koero Mkundi said...

Kaka Bwaya, kwa kuangalia tu Historia ya hapa Nchini, hivi ni kabila gani linasifikia kwa wanaume wao kuwa na Nguvu za kufanya kazi? Bila shaka ni Wanyamwezi na Wasukuma, Je wakijua chakula chao kikuu?
kaka Matondo nisaidie.......
kaka Bwaya Ugali Uliopikwa na Msukuma au Mnyamwezi ni mgumu kama jiwe na ndio maana walichukuliwa Manamba kwa wingi kwenye mashamba ya mkonge na mashamba ya Miwa.
Nenda Tanga au Kilimanjaro na kwingineko kunakolimwa mkonge au kwenye mashamba ya miwa utawakuta wamejaa tena kwa idadi ya kutosha.
Kaka Bwaya Iwapo Binti yako ataolewa na Msukuma au Mnyamwezi basi hatakufa njaa Bro.....LOL
Bado natafakari sifa za hao watangaza nia wawili.......

September 17, 2010 5:22 PM

Ramson said...

jamani na mie naomba nijiunga na kinyang'anyiro, mweh! unajua sifa ya mwanamke mzuri huwa anagombewa...LOL
Haya Koero andaa uwanja wa kuonyeshana ubabe mie naahidi kumaliza ugali kilo moja

September 17, 2010 5:24 PM

Markus Mpangala said...

Mtani wangu Fadhy una mkwara weyeeee, lakini mimi nasema hivi, raha ya ubwabwa utandu, utamu ukizidi sema bandu bandu......
Najieleza kama sinema ya kihindi, lakini kumbuka bila mimi kuandika pale KIJIJINI kwangu hata Koero asingeliandika.
Najieleza, na nimemtumia ujumbe chonde mtose mtani wangu fadhy, nipe mie hilo jambia la maisha yako nilishike nikulinde.
Koero napiga MAGOTI NIPO CHINI YA MIGUU YAKO. NAOMBA TUOANE. ila naomba usiseme mie mtangaza NIA.
nimekuja tayari naomba TUOANE

September 17, 2010 5:25 PM

Yasinta Ngonyani said...

Mie yangu macho nasubiri mshindi, ili tunywe ugimbi na kucheza limgambusa na lizombe....kaazi kwelikweli

September 17, 2010 5:53 PM

chib said...

Kwi kwi kwiiii, nakushukuru Koero kwa kutufanya tuhamie huko wanapopaita busy kwa msongo wa mawazo. Mie nipo tayari kumpa tiba ya kisaikolojia atakayeangukia pua kwi kwi kwi

September 17, 2010 6:52 PM

Fadhy Mtanga said...

nasema hivi Koero huyo mtani wangu shemeji Markus hana lolote. waswahili wanasema chema chajiuza, kibaya chajitembeza.
huyo jamaa hapo hana lolote ndo maana anatumia maneno mengi akisahau kuwa barafu haijengi nyumba.
maneno matupu hayavunji mfupa.
kwanza huyo jamaa ni mvivu sana Koero. halafu hajui kujali. kama anabisha mwambie aniruhusu niseme kisa cha yeye kufukuzwa kwa kimada wake wa awali.
mie wala sihitaji kumpaka matope ili nishinde kwani najua tayari wewe ni wangu na hivi karibuni nitakwenda kumsabahi bibi Koero.
ninachague mimi kwa kuwa ninastahili kuwa wako.

September 17, 2010 6:57 PM

Markus Mpangala said...

Wakati naandika pale KIJIJINI kwangu nilifanya tafakuri anuai. najua mtani wangu fadhy nitakufichulia hapa hapa.
Koero weweeeeeeee ebu angalia pale KIJIJI kwani kuna watu wawili wanatembea kwa mahaba wameonyesha migongo. halafu muulize mtani wangu fadhy wale ni nani.
Kama ni wako basi anakudanganya,hakujali anakuzuga na busu la alfajiri, lenye ukakasi anuai.
NIPE MIMI, kwani sifanani na stori za makande ya saidi mnyamwezi na mipasho ya wazua methali.
NIPE MIMI ila usinihurumie.
Ramson ni kijana wa hadaa, anaweza kukupeleka kuzimu bureee.
NIPE NIPE NIPE MIMI MIMI
kama sukari nitalamba na asali nitaonja. ujumbe na radha vyote ni vyangu pomoni mdomoni. Koero KWAKO SISEMI WALA SIHEMI..... najua mtani wangu fadhy anakupa maneno machache lakini mimi nakupa mengi kwakuwa najua UTAMU WA PENZI NI MANENO MURUA yenye kila viungo vya STORI ZA MAKANDE zisizo na umahiri wa kusimulia kitakatifu.
PENZI akupaye ni yule aimbaye kwa lugha tamu ya MAHABA ile lugha ya kuomba ridhaa, ile lugha ya kukata rufaa, ile lugha ya kuimba kihindi au kunena kwa lugha. kumbuka NITAKUANDIKIA TENA PALE KIJIJINI KWANGU jinsi unavyonikorohua nafsi.
Mtani wangu Fadhy; dume lenye uhakika halimchungulii mkewe...... inakuwaje ukaombea kitoweo chako kwa jiraniiiii....... haya twende na stori za makande zipo kuleeeeeeeee eee

September 17, 2010 11:29 PM

Fadhy Mtanga said...

mie si fundi wa maneno kwa kuwa si mwanasiasa kama mtani wangu na shemeji yangu Markus.
ila tu nakupa angalizo, ndoa siyo majaribio kama mashindano ya mpira ama michuano ya urembo. kama utaamua kuijaribu ladha ya ndoa iliyoshindwa, basi ambatana na huyu kijana shemeji yangu.
unakijua kisa cha mie kuamua kumwita jina la shemeji kama nyongeza ya jina la mtani?
angalizo jingine, huyu jamaa anatokea lile kabila ambalo ukiwapa pesa wanafikisha kwa uaminifu, ukiwapa........utavuna mabua.
kama kawaida mie siongei sana kwa kuwa najua ushanichagua.

September 18, 2010 12:07 PM

Markus Mpangala said...

Mtani wangu shemeji yangu duh!!! uliwaza nini na wakinipa nini mweeeeeeeeeeeee rahaaaaa si unajua ukipewa kwa ridhaa wala hukati rufaa, bila chambi chambi au? Mtani una mamno weyeeee, lakini najua STERINGI ANAKUFA PICHA NDIYO INAANZA. Koero NIPE MIMI

September 18, 2010 2:00 PM

John Mwaipopo said...

utani utani mara mmoja wao anachukua

September 18, 2010 4:07 PM

Chacha o'Wambura a.k.a Ng'wanambiti! said...

mmmh!

September 18, 2010 5:09 PM

Anonymous said...

Sasa mimi kama mzee mzima, inabidi nitumie busara kuweka mambo kwenye mzani.
Napenda kujua ni nani ni bachelor au spinster kati ya wachangiaji hawa hapa ili niweze kutegeu kitendawili hili, Kusema ukweli Koero amenipa mtihani mgumu katika mada zaka zinazofanana na hili. Hapa lazima jambo lifanyanyike! Binafsi najitolea kuwa mwamuzi au refari kwa lugha ya kisoka.

September 18, 2010 6:08 PM

Markus Mpangala said...

Kaka Mwaipopo hakika SITANII naomba niwie radhi ukidhani huu ni UTANI, hakika mie toto la kinyasa sina neo jingine zaidi ya KUMPENDA KWA DHATI binti Mkundi.
Nipo kwa shida na raha, utamu wa penzi ni ridhaa na raha murua, Najua kuwa penzi Muwali ndilo hulizala AU tamu ya HUBA na maisha ya ndoa adhimu,
ni raha kumtakia UMPENDAYE TOKA MOYONI hakika sina jingine nipe raha na amani Koero tafadhali Koero. sina chambi chambi wala jembe la la kuchimbia harara bali NIMEUMBWA na harara zenye kila aina ya MANUKATO YA PENZI....
Koero mwana wa Mkundi, nipo makini ninenacho wala sitangazi nia hapa bali dhamira ya KUISHI NAWE DAIMA. kwa kweli ningeweza ningekupa mlima Kilimanjaro, lakini hadidu rejea nitakupa MOYO wangu uchukue UINGIE ndani uone PENZI LANGU..... Mtani wangu shemeji usiniwekee kiwingu maana wanipa jakamoyo ...
Koero sina AMALI nitakupa HUBA KAMILI.

September 18, 2010 7:35 PM

Fadhy Mtanga said...

Mpenzi Koero,
Usimsikilize Markus,
Hajiamini kajaa wasi,
Bure ajitakia kesi,
Saizi yako hajaifikia.
Koero nichague mie,
Ili maishani nikufae,
Matamu nikupatie,
Mapenzi ya kufurahia.
Markus atakupoteza,
Mrembo atakuchakaza,
Kwangu utakula utasaza,
Na afya njema pia.
Mie kutunza najua,
Kwa Markus utaugua,
Kijana atakusumbua,
Uteseke na dunia.
Mpenzi wewe ni wangu,
Ua la ulimwengu,
Markus aondoe kiwingu,
Najua ushanichagua,
Mtani nakupa tu pole,
Rudi katafute wale wa shule,
Mfupa umekushindale,
Mwenye meno ukaniachia.
Koero mrembo Koero,
Markus kajawa kihoro,
Atakulisha wewe kiporo,
Ni mvivu kujitafutia.
Nashukuru umenielewa,
Nami umeshanichaguwa,
Raha tele utapewa,
Raha iliyozidia.
Wasalaam mpenzio,
Kijana Fadhy.

September 18, 2010 8:33 PM

Markus Mpangala said...

Najua dhima ya penzi
koero daima nitakuenzi,
penzi zaidi ya enzi,
sisemi wala sihemi,
Koero binti mkundi,
mrembo unipaye amali,
nikuonapo hakika silali,
katu nitakuoa ewe mwenzi

September 19, 2010 5:27 PM

Fadhy Mtanga said...

Katu nitakuoa ewe mwenzi,
Kiswahili tu hakiwezi,
Atakuletea jinamizi,
Usiku kucha kukusumbua.
Koero tafakari hilo vema,
Kumtosa ndiyo hekima,
Markus kamwe si mwema,
Kila siku utalia.
Huyo mwanaume suruali,
Hawezi kuvunja majabali,
Utalala na njaa ile kali,
Mrembo mwiliwo kupungua.
Markus anajua tu kuchonga,
Maneno mengi achonga ngenga,
Si mume bali kibaramchanga,
Ukweli sasa ninakwambia.
Mwanaume gani chaukarange,
Anaendeshwa na nazo bange,
Hakufai huyo umpinge,
Njoo kwangu mtoto ukatulia.
Wewe ndiwe ua lilochanua,
Markus hajui hata kumwagilia,
Ukimkubali mbona utalia,
Njoo kwangu utafurahia.
Markus nasema hatokufaa,
Utakonda mrembo ukasinyaa,
Njoo kwangu hakika utang'aa,
Maana najua kuhudumia.

September 19, 2010 6:34 PM

Koero Mkundi said...

Ha ha ha ha haaaaaaa..... naona mpambano umefika patamu...duh! hadi Mashairi! hakika Ngoma inogile mwayego.....LOL
Haya waungwana kuna marekebisho kidogo ya masharti ya kumpata kimwana mie Koero Binti Mkundi.
Ngoja nifanye summary maana ni marefu kweli kwani mzee mkundi anataka kuhakikisha kuwa naangukia katika mikono Salama.
Nipeni muda nitaweka bandiko hivi punde na hilo ndilo litakalotujuza mshindi......LOL

September 20, 2010 12:34 PM

Markus Mpangala said...

Mtani huniwezi,
upupu au kwenzi,
dola au dinari,
pauni au shilingi,
nalijua penzi,
lile muwali,
daima nilienzi,
Mtani wajua mepes,
wajua ile sentesi
kwangu ni parandesi,
hadidu zaidi ya fenesi,
Fadhy mwana wa Mtanga,
hujui kulea kimwana,
punguza lukuma,
wajua toto la kinyasa,
daima uvivu lakana,
chambichambi,kukusanya,
siyo wewe mwana bodaboda,
kila siku kiguu na njia,
Tramp wasafiri kumwacha mwana,
baridi kujiumizia,
katu siyo mume wa maana,
kivuli watembelea,
ati kujitafutia,
ukwasi haujengi penzi,
ukata haujengi penzi,
Koero nipe penzi,
Mtani hatakuenzi,
FADHY MTANGA a.k.a shemeji mtani wangu daima
nisikize kiinglishi, mwana naonngeza kubonga,
sina bichikoma,
navaa tu bugaluu sana,
Eti mtani wangu....
Shall i campare the to a summer's day?
Thou art more lovely and more temperate;
rough winds do shake the darling buds of may,
and summer's leave hath all too short a date.....
Koero binti mkundi,
wajui ninalo penzi,
hakika nienzi...

September 20, 2010 12:47 PM

Markus Mpangala said...

sentesi ya kwanza nimekosea mtani wangu, inasema Shall i compare thee to a summer's day?

September 20, 2010 12:51 PM

Fadhy Mtanga said...

leo nimepita tena hapa na kuangua kicheko vibaya mno. katika kublog kwangu, hii ni posti iliyonivunja mbavu kila nikija kusoma na kuacha maoni...
sisi wote watatu, koero, markus nami ni marafiki wazuri sana.
ahsante sana Koero kwa kuchngamsha umati.

November 19, 2010 10:23 PM

Fadhy Mtanga said...

Jamani Koero mbona umeadimika hivyo?

August 23, 2012 7:55 PM

Mwalimu Nyerere aliona mbali

$
0
0

mwalimu nyerere

14 OKTOBA 1999, Tanzania, Afrika na dunia nzima ilipatwa mshituko baada ya kutangaziwa kuwa mwanamapinduzi na mpigania haki na usawa duniani, baba wa taifa la Tanzania, mwanaAfrika mzalendo wa kweli, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ameaga dunia huko katika hospitali ya Mt. Thomas, Uingereza alikokuwa akitibiwa.

Leo ni miaka 13 sasa.  Taifa na wapenda haki na uadilifu wote duniani tunamkumbuka.  Alikuwa mwalimu wa kweli.  Mwana wa kweli wa Tanzannia na Afrika.

Tunapomkumbuka, ningependa tujikumbushe mambo mawili aliyoyazungumza panapo Machi 13, 1995 alipokuwa akizungumza na Klabu ya Waandishi wa Habari Tanzania.  Mwalimu, pamoja na mambo mengine mengi ya msingi, alizungumzia rushwa na muungano.

Kuhusu rushwa, katika mengi aliyoyazungumza, pia alisema;

‎"Serikali ya wala rushwa haikusanyi kodi. Itabaki kufukuzana fukuzana na vijitu vidogo vidogo mabarabarani hivi tu basi. Hili jambo ni sheria kama ile ya kwanza niliyowaambiwni kuhusu ubaguzi, mkianza ubaguzi, mtaendelea moja kwa moja; hamna mahali pa kusema simama hapa. Mkisha kuwa wala rushwa, mtaabudu wenye mali. Mimi ni Mkristu, sijui Kuruani inasema nini, lakini msahafu wa Kikristo, Injili, ambayo na Waislamu wanamkubali Nabii Issa, kwa maneno yake mwenyewe "huwezi kutumikia mabwana wawili, mmoja fedha, mwingine Mungu; haiwezekani, utachagua katika wawili hao".

Akazungumza pia kuhusu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambao umekumbwa na misukosuko kadhaa wa kadha kutoka kwa watu wasioitakia mema nchi yetu.  Mwalimu Nyerere akazungumza mambo mengi sana, kati ya hayo, akasema;

‎"Watu wazima wamezungumza Muungano, kwamba tuuvunje au tuendelee. Ilikuwa ipo hatari ya kuvunjika na wala haijaisha. Watu wamezungumza Uzanzibari, na baadhi ni viongozi wetu, wanajivunia Uzanzibari. Nadhani wengine wanafikiria hata kujitenga. Wapo si wengi; lakini wapo. Kujitenga maana yake ni kuvunja nchi ivunjike tusiwe na nchi moja, tuwe na nchi mbili. Ni jambo linalozungumzwa. Tunataka kiongozi na viongozi watakaoelewa hivyo. Huku kuzungumza Uzanzibari si fahari. Si jambo la fahari. Hatima yake tutavunja nchi. Zanzibar, mtu mwenye akili hawezi kufikiri Uzanzibari ni fahari: hana akili.


Hawezi akautukuza Uzanzibari kwa kujiita 'sisi Wazanzibari' na 'wao Watanganyika'.


Nadhani ile ina usalama ndani yake. Kwamba Uzanzibari ule, Utanganyika ule una usalama ndani yake. Hatima yake Zanzibar itajitenga. Zanzibar ikijitenga kutokana na ulevi tu; sisi Wazanzibari na wao Watanganyika wakumbuke kwamba Muungano ndio unaowafanya wanasema 'sisi Wazanzibari' 'wao Watanganyika'. Nje ya Muungano, hawawezi kusema hivyo: kuna 'wao Wapemba' na 'sisi Waunguja'.


Nataka mjue hivyo. Nje ya Muungano hakuna 'sisi Wazanzibari' 'wao Watanganyika'. Hakuna. Kinachowafanya mjiite 'sisi' ni ubaguzi wa kuwabagua Watanganyika. Wakiisha kuwabagua Watanzania Watanganyika, ile dhambi ya ubaguzi, haifi inaendelea. Dhambi ya ubaguzi ukisha kuitenda inaendelea: ni kama ukila nyama ya mtu utaendelea kuila. Mtamaliza mtatengana na Watanganyika halafu, mara mtakuta kumbe 'sisi' 'si Wazanzibari'. Kuna 'Wapemba' na 'Waunguja'. Wapemba watapata msukosuko kidogo aaolololo!


Mtakuta kumbe kuna Wazanzibari na Wazanzibara! Hamtakaa salama. Hamwezi mkakaa salama baada ya kutenda dhambi ya kuwabagua watu wa nchi yenu ile ile moja mkawaita 'wale wao' na 'hao sii'. Dhambi ile haiishii hapo. Ndivyo historia ilivyo; ni sheria ya historia siyo sheria ya Mwalimu Nyerere. Huwezi kufanya ubaguzi wa namna hiyo halafu dhambi ile ikuache hapo hapo. Hapana itakuandama."

Hivyo ndivyo ninavyomkumbuka Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (1922-1999) kwa siku ya leo.

Tafakari!

Mwenyezi Mungu akupumzishe kwa amani.  Amina.

Hawa watu!

$
0
0
KATIKA kupitia pitia historia barani Afrika nimekutana na mambo kadha wa kadha ambayo yameniacha kinywa wazi mara chungu mbovu.  Haya ni baadhi.

Mohandas Karamchand Gandhi (Mahatma Gandhi) wakati huo akiishi Afrika Kusini alikuwa mpigania haki ambaye utawala wa kikaburu ulimwona gaidi.  Leo hii ni binadamu anayeheshimika mno ulimwenguni kama mtu mwema aliyepata kuishi.

Samuel Daniel Shafiishuna Nujoma (Sam Nujoma) wakati huo akiwa mkimbizi akikimbia kimbia kupitia Zambia na Tanzania kwa kuonekana gaidi na mchochezi asiyetakiwa kabisa na makaburu wa Afrika Kusini waliokuwa wakiitawala Namibia (South West Africa).  Leo hii ni moja ya Waafrika wanaoheshimika zaidi kama alama ya uhuru wa Afrika.

Nelson Rolihlahla Mandela, huyu kila mtu anazifahamu habari zake.  Namba moja katika listi ya magaidi waliokuwa wakisakwa kwa udi na uvumba na CIA (si mnawafahamu vurugu zao katika bara la Africa wakati wa Negritude?) na miaka 27 akiwa kifungoni katika gereza tata kisiwani Roben.  Leo hii ni namba moja katika orodha ya Waafrika wanaoheshimika zaidi ulimwenguni.

Samora Moisés Machel, huyu naye Wareno waliokuwa wameigeuza Msumbiji kuwa jimbo lao barani Afrika walimwona kama gaidi na mchochezi asiyefaa kabisa kuishi.  Leo hii Msumbiji na Waafrika wengine wanamwona kama mkombozi wa kweli na shujaa wa taifa la Msumbiji.

António Agostinho Neto huku kama Machel tu.  Wareno waliojimilikisha Angola walimwona vile vile kama walivyomwona Machel.  Leo hii ni alama ya uhuru wa Angola.

Jomo Kenyatta alishitakiwa na wakoloni Waingereza kwa makosa ya ugaidi na uchochezi.  Akafungwa.  Leo hii huwezi kuitaja Kenya huru bila kulitaja jina lake.  Anaendelea kuheshimiwa na vizazi vyote, si Kenya tu.

Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, hakuna mtu asiyemfahamu.  Wajua habari zake?  Wakati wa ukoloni wa Mwingereza alishitakiwa kwa makosa ya uchochezi.  Isingekuwa msaada wa rafiki zake, mawakili wa kizungu ilikuwa aende jela.  Huyu ndugu, leo hii ni moja wa Waafrika wanaoheshimika zaidi siyo tu Afrika, bali duniani kote.

Hawa wote, wakiwa ni baadhi tu ya wale niliokutana nao katika makaratasi yangu yalioandikwa matukio ya kihistoria walikuwa binadamu wa pekee mno.  Binadamu waliokuwa na dhamira safi mioyoni mwao juu ya watu waliokuwa wakiwaongoza.  Watu hawa ni mfano halisi wa kuwa lila na fila kamwe havitangamani.  Walisemewa maneno ya uongo.  Walitungiwa kesi.  Wakalazimika kuwa wakimbizi wakati mwingine.  Wakateseka kwa kiwango kikubwa mno.  Lakini si punde, ukweli ukajulikana.  Dhamira zao zikaonekana dhahiri.  Basi, raha, kheri na fanaka vikawa kwa wale waliokuwa wakiwaongoza.

Historia.  Mwalimu wangu mmoja alipenda kusema historia hujirudia.  Mi bado sijui.  Siijui vema historia.  Ningali nikijifunza.  Nina vitabu vya aina mbili.  Vilivyoandikwa kwenye makaratasi.  Vingine ni vile ambavyo havijaandikwa, bali navishuhudia.

Nimalize kwa kumnukuu mwanafasihi Ebrahim Hussein, "Wakati Ukuta."

Jumapili njema.

Porojo za leo: Mei Mosi!

$
0
0

MWANANCHI mimi naamshwa kutoka usingizini kwa mlio mkali wa simu yangu ya Kichina.  Simu inalia kweli utadhani imefungwa sub-woofer.  Nakwambia ukubwa wa muziki wake usiombe mtu akupigie simu ukiwa kwenye ibada ama kikao nyeti kweli.  Unaweza tamani ardhi ipasuke walahi vile.  Naitazama simu ili kumfahamu mpigaji.  Naona namba tu.  Nani tena huyu wa kunipigia simu asubuhi yote hii wakati mie nataka kufaidi usingizi wa siku ya mapumziko.  Naamua kuipuuza.  Navuta shuka na kugeukia upande wa pili.

“Ndugu yanguuu tizama unakokwendaaaa…vile vile ukumbuke ulikotokaaaa….”  Simu inaita tena.  Najua vijana wa siku hizi hamuwezi kuufahamu huu wimbo wa mkongwe Marijani Rajab.  Nyie zenu ni hizi bongo fleva ambazo mnachezea mabinti wa watu na kuwabadili kama nguo halafu kila mkiacha mnatunga nyimbo ili muuze.  Kweli dunia imebadilika sana.  Watoto wa siku hizi adabu wala hakuna.  Kila mtu anajifanya ‘machi noo’.  Vijana ni vurugu kwa kwenda mbele.  Mambo ambayo zamani yalifanywa na wanyama sasa ndo yanafanywa na vijana wetu.  Taabu kweli kweli.

Hee!  Kumbe simu bado inaita.  Naitazama tena.  Namba siifahamu.  Naamua tu kuipokea maana itakuwa kero tupu.  “Haloo!”  Naitikia kwa sauti nzito utadhani nimekabwa na fupa la kuku wa kienyeji kooni.

“Mwananchi wewe upo?  Jamani mbona umekuwa adimu hivyo yakhe utadhani miguu ya nyoka?”  Asalaleeh!  Ni yule yule rafiki yangu wa Unguja.  Leo sijui kawaza nini kunipigia simu maana sijazungumza naye karibia mwaka.

“Asalaam aleykum maalim wangu!”

“Waleykum salaam!  Kitambo sana sheikh wangu.  Madhila gani yamekusibu hata ukapotea usisikike tena?  Hata kun’julia khali huna mpango.  Ama ndo mambo ya kamisheni hayo yanakufanya un’sahau mie?”  Keshaanza.  Si unamfahamu huyu jamaa huwa haishiwi maneno?  Sijui leo kaja na lipi maana huwa hapigi simu ilimradi tu.

“Maisha tu ndugu yangu!  Pilika zimekuwa nyingi kuliko uwezo wangu.”

“Sijawahi kukuona ukiishiwa utetezi.  Nilimiss sana maneno yako ya shombo ntu wewe!  (Hee!  Kumbe nna maneno ya shombo, hata sikufahamu, haya makubwa!)  Mambo mengi yanatokea nilitamani kukusikia ukisema!”  Walau leo anazungumza kwa vituo.

“Kama yapi ndugu yangu?”  Namwuliza maana’ke asije nitia maneno bure ilhali sikusema.

“Ina maana pilika ni nyingi hadi huyaoni?  Huoni komedi shoo mpya pale Dodoma?”

“Kuna nini kwani?  Hata sina habari!”  Namzuga maana sitaki kujadili mambo ya kunipa stress asubuhi yote hii!

“Tuyaache hayo ntakupigia siku nyingine.  Leo nimekupigia kuhusu Mei Mosi.  Vipi kuna uwezekano wa kupandishiwa mishahara kweli.  Nimesikiasikia tu tetesi.!”

Hapo ndipo aliponikuna.  Nikainuka na kutupa shuka kule.  Nikaketi kitako.  “Kupanda kwa mishahara?  Walahi vile ndugu yangu mie kichwa kinazidi kuniuma tu hapa!”

“Kwa nini kikuume?”

“Sasa kama gharama za maisha zinapanda kila siku unadhani huo mshahara ukipanda unaleta unafuu.  Hizo ni hesabu tu za kujumlisha na kutoa.  Ni sawa na una kumi halafu unajumlisha tano kisha unatoa ishirini.  Unadhani utabaki na kitu gani?”

“Sasa hapo mwananchi wewe si unabaki na deni la tano!”  Nikajibiwa.

“Ahaaa!  Kumbe unajua hesabu.”

“Unamaanisha nini hapo sasa maana nawe kwa mafumbo utadhani….”

Nikamkatisha.  “Siyo mafumbo.  Linganisha kupanda kwa gharama za maisha na kupanda kwa hicho kipato.  Maisha yanazidi tu kuwa magumu.  Pesa zimejenga uadui na mifuko yetu.  Ukiziweka tu wala hazitaki kukaa.    Yaani maisha haya full kizungumkuti!”

“Sasa unadhani nini kifanyike?”

“Mambo ya kufanyika yapo mengi!  Mi nadhani la muhimu zaidi rasilimali za nchi zilindwe vema kwa uaminifu.  Kila kitu kifanyike kwa uadilifu ili tufike mahali tujimudu kiuchumi.  Tatizo siyo mishahara mikubwa.  Tatizo ni udhibiti wa mfumuko wa bei.  Hiyo mishahara hata ikipandishwa kila siku kama mfumuko wa bei haudhibitiwi ni kazi bure tu.  Maisha yanazidi kuwa magumu sana.  Pesa inadhidi kukosa thamani.  Si umeona mwenyewe nauli zilivyopanda.  Zimepanda mno.  Sasa unadhani mishahara ikipandishwa inaleta utofauti gani wakati bei za bidhaa zote inapanda?  Sema mwenyewe usije sema mie nna maneno sana!”  Nikameza mate.

“Mmh!  Ila nalo neno maalim wangu!”

Tii ti tiii!  Simu ikakatika.  Sijui kaishiwa salio!  Nikajitupa tena kitandani na baridi hili tena!

Heri ya Mei Mosi!

Sisi tu wamoja

$
0
0

ASUBUHI ya leo ninapokutana na  habari za kanisa
kulipuliwa najikuta nikitafakari miaka kadhaa
nyuma. Ninatafakari huku nikisononeshwa na
jamii yetu inakoelekea, hususani mipasuko ya
kidini.

Ninajaribu kuwatazama ndugu zangu ambao
tumechanganya sana hizi imani kuu mbili hapa
Tanzania. Mwingiliano wetu ni mkubwa kiasi
kwamba huwa hatuoni tofauti miongoni mwetu.
Tofauti pekee ambayo huonekana ni kuwa wapo
wanaokwenda nyumba za ibada siku ya Ijumaa,
ilhali wengine wanakwenda siku ya Jumapili.
Tofauti nyingine, labda ni matumizi ya lugha.
Msamiati. Wakati wengine wanasema kuswali,
wengine wanasema kusali.

Leo pia nimepata kutafakari wakati wa kukuwa
kwangu, hususani angali nikisoma elimu ya msingi
na sekondari. Nilipata kuandika ile siku ya mwisho
ya mwaka 2012. Wakati nakuwa tulikuwa tukiishi
mji mdogo wa Tunduma mkoani Mbeya. Mtaa
wetu ulikuwa na nyumba nane. Familia hizi nane
zilikuwa ni mchanganyiko wa dini zote mbili.
Uislamu na Ukristo. Zile za Waislamu zilikuwa na
Wakristo ndani yake, vivyo hivyo kwa Wakristo.

Nilipata kueleza mara nyingi kuwa toka tukiwa
wadogo tulielekezwa kuishi maisha ya kuamini sisi
sote tu wamoja. Ukifika wakati wa Eid ama
Maulid, sote tulikula pilau pamoja. Familia za
Kiislamu zilipika chakula na kualika familia zingine.

Baada ya chakula cha mchana, tulichukuana
watoto wote hadi ng'ambo, nchini Zambia,
kwenye mji wao wa Nakonde. Huko tulitembea
pamoja, kwa furaha na upendo mkuu. Kisha,
nyakati za jioni tulipenda kwenda sinema pale
Tourist Hotel, almaarufu kwa Shams. Saa moja
jioni ilitushuhudia sote tukirejea mtaani kwetu
kwa upendo na umoja wa aina yake.
Utamaduni huo uliendelea kipindi chz Noeli na
Pasaka. Sote tuliyafurahia maisha hayo.

Maisha hayo yalinijenga kimtazamo kuwa sisi ni
wamoja. Sisi ni wamoja. Nitaamini hivyo hadi siku
Mwenyezi Mungu atakaponiita.

Kwa nini leo ninayaandika haya? Ninayo sababu
moja kubwa. Ninapenda jamii yangu iamini sisi ni
wamoja. Tofauti zetu ni tofauti za kihistoria tu.
Ninasisitiza hilo. Tena tofauti hizi wala
hazikutokana na utashi wetu. Nisiende sana huko.

Maisha yangu yamenifundisha sisi ni wamoja.
Familia ninayotoka imenifundisha kuwa sisi ni
wamoja. Toka nikiwa mdogo hadi dakika hii
niandikapo makala haya, nimekuwa na bado
ninazungukwa na marafiki wa imani hizi zote
mbili. Tunapendana kwa dhati. Tunaaminiana.
Tunathaminiana. Tunaheshimiana. Tunasikilizana.
Tunasaidiana.

Huwa nasema mara nyingi. Nirejee leo. Maisha
yangu yamenifundisha kutouliza dini ya mtu
kama sababu ya jambo lolote katika kuhusiana
nami na mtu mwingine. Sina sababu ya kufanya
hivyo kwa kuwa ninaamini sisi sote tunamwabudu
Mungu mmoja.

Wakati jamii yetu ya Kitanzania ikizidi kuzama
katika shimo la sintofahamu ya kidini, nimependa
asubuhi ya leo, kuitumia kalamu yangu
kuwaambia Watanzania wenzangu, sisi ni wamoja.

Waama, sisi ni wamoja.

Amani iwe kwenu nyote.

Fadhy Mtanga,
Sinza, Dar es Salaam.
Jumapili, Agosti 25, 2013.

Porojo za leo: Magumashi magumashi tu sebuleni hadi jikoni!

$
0
0
“NATAKA kulewaaaaa…..lewaaa….nataka kulewaaaa…..lewaaa….nikizidisha nimwage radhi..!”  Unaweza ukadhani mwananchi mie nimepatwa na wazimu.  Huchelewi kuwapigia simu nduguzo na kuwaambia, “Mwananchi yeye hakya nani Mungu na mtume vile siku hizi amekuwa pampula hadi anaimba nyimbo hadharani kusifia upampula wake.”  Halitokuwa kosa lako.

Kama hufahamu ndo nakufahamisha.  Huo ni wimbo wa kwenye simu yangu inapoita.  Ukisikia sauti tamu ya yule mkazi wa zamani wa Tandale halafu akahamia kule Mbagala ambako nyumba yao ilikuwa mbele ya jalala, basi ufahamu kuwa simu yangu  ndo inaita.  Tena Mchina wangu ulivyo na jisauti kiburushuti kama limefungwa sabuwufa, walahi vile utatamani nisipokee haraka ili  uendelee kufaidika na burudani ya sauti muruwa kutoka kwa kijana aliyeambiwa na wazee wake wa zamani kuwa kazi na dawa!

Unaona sasa?  Nanogewa na stori hadi nasahau kuwa simu yangu inaita.  Naichukuwa simu haraka haraka utadhani ninaogea kibarazani kisha nikasikia hodi.  Kumtazama tu mpigaji, najikuta nashikwa na kicheko.  Ni yuleyule swahiba wangu wa Unguja.  Sijui leo ana nini la kuniambia maana sijazungumza naye kitambo kirefu kweli kweli.

“Asalaam aleykum!”  Naanza kwa mbwembwe zangu.

Haraka haraka anaitikia.  “Waleykum salaam mwananchi wewe! Kimya nno ndugu yangu  utadhani tuligombana.  Toka n’seme tunataka Zanziberi yet undo hutaki hata kuwasiliana nami? Vibaya hivyo ndugu yangu.  Sisi ni wamoja kabisa kabisa hakuna haja ya kuchukiana!”

Kama unakumbuka vema, sifa ya huyu swahiba wangu ni kuwa akishaanza kuongea hakupi nafasi.  Anaongea mfululizo utadhani kamezeshwa memori kadi ya jibii alfu lela.  Mi namsikiliza tu.

“Usinifanyie hivyo ndugu yangu.  Wajua kabisa nikitaka msaada wa mawazo hususani kwenye mambo ya masheria haya huwa naja kwako!”

Naamua kumkatisha.  “Nipo ndugu yangu wala sijakupotezea.  Pilika tu za jiji hili hazinipi fursa ya kupumzika.  Afadhali umesema kuwa sisi ni ndugu zenu.  Sasa kama ni ndugu zenu mbona mwapigia debe kutukimbia?”

“Ushaanza mambo yako.  Leo sitaki tujadili hilo.  Maana huchelewi kunilainisha nikalainika.  Leo nataka tujadili mambo mengine kabisa.”

“Yepi hayo maalim wangu?”  Nikamwuliza.

“Hayo mambo ya sebuleni na jikoni!”  Akanijibu haraka haraka utadhani anatokwa roho.

“Sebuleni na jikoni?  Mbona sikuelewi ndugu yangu?”

“Tatizo lako una haraka sheikh wangu.  Punguza wahka moyoni.  Sebuleni ni pale Dodoma kwenu pale.  Ushan’fahamu mwananchi weye?”

“Bado kidogo!”

“Nawe umekuwaje siku hizi?  Mgumu kweli kuelewa.  Nazungumzia pale mjengoni.  Pale kwa watunga sheria.”

“Ahaa!  Unazungumzia ukumbi wa vurugu-mechi kumbe?  Ha ha ha ha haaaaa!  Ngoja nicheke kwanza mwananchi mie.  Nilikuwa naona tu katika Al-Jazeera mambo kama hayo yakitokea huko Bara Asia.  Labda kidogo kwa jirani zetu Wakikuyu.  Si punde nasi tumeyashuhudia.”

“Nafurahi sasa umenielewa. Hivi unajua tatizo ni nini?” Akaniuliza swali utadhani mie ndo niliyeuanzisha mjadala huo.  Kabla hata sijafahamu nimjibu nini, akaliendeleza.  “Tatizo ni upeo mdogo wa tuliowaamini kutuongoza.”

“Unamaanisha nini swahiba?”  Nilihisi simwelewi.

“Nyumba huwa haivurugwi na watoto hata siku moja.  Nyumba huwa inavurugwa na baba anayeshindwa kuiongoza vema familia yake.”

“Mmh!  Sitii neno!”

Akawaka. “Una lipi la kuzungumza hapa wewe?  Nyie watu wa bara sijui vipi samtaims?  Busara tu zinawashinda wakati mwingine.  Kuwa kiongozi maana yake siyo kuheshimiwa.  Maana yake ni kuheshimika.”

“Tuyaache hayo ndugu yangu.  Na jikoni ni wapi?”  Nikamwuliza.

“Mwone kule.  Najua una sababu zako ndiyo maana unakwepa tusijadili vurugu-mechi zisizo na kichwa wala  miguu.  Na ujanja wako wote nikisema jikoni bado huelewi? Jikoni ni pahala panaposongwa ugali.  Unajua nini kinatokea sasa?” Akahoji.

“Hapana!”

“We bogasi kweli mwananchi wewe!”  Nikatamani kumjibu, nikamkaushia.  Akaendelea.  “Wenzako siku hizi wamelifanya taifa hili kuwa la wasonga ugali.  Kila siku habari ni zao tu mchana kutwa, usiku kucha wanahangaika tu na viroba vya sembe.”

Nikamwelewa.  “Unajua inasikitisha sana ndugu yangu.”

“Lazima isikitishe sana.  Taswira ya nyumba yetu inazidi kuchafuka kila uchao.  Dunia nzima sasa wanatujua sisi ni wabeba sembe.  Umesikia jana tena wameipiga kiberiti meli iliyokuwa imepakia sembe la kutosha.  Meli ya kwetu ile.”

“Nimesikia ndugu yangu.  Tena nasikia imesajiliwa huko huko kwenu mnakotaka kutukimbia.”

“Achana na kauli zako hizo sheikh wangu.  Haijalishi imesajiliwa wapi sote tunachafuka.  Ndiyo maana nakwambia nchi hii imekuwa magumashi bin vurugu-mechi sebuleni na jikoni!”

“Ha ha ha ha ha ha ha haaaaaaa!  Nicheke miye!  Sicheki kwa mazuri bali huzuni tele moyoni!”

Akadakia.  “Inatia hasira.  Inatia simanzi vijana wetu wanaharibika kila siku.  Wenyewe wamekaa kimya.”

Ti ti tiiiii!  Simu ikakatika.  Atakuwa kaishiwa salio huyo.

Ila kaniachia tafakuri.

Magumashi bin vurugu-mechi.

Sebuleni na jikoni!


Mwananchi mimi,
Fadhy Mtanga,
Kariakoo, Dar es Salaam.

Jumatatu, Septemba 9, 2013.

Majina ya kusisimua ambayo watu wamewahi kupewa duniani

$
0
0
Ushawahi kusikia majina yenye kusisimua?  Bila shaka umekutana nayo mengi katika jamii yako.  Kwa mfano, katika jamii ya Kitanzania tumekwishakutana na majina kama Kibakuli, Siogopi, Sinataabu ama hata Ngonjera.  Kwingineko duniani, hali ni ile ile.  Yafuatayo ni majina ya kusisimua ambayo watu wamewahi kupewa duniani.

1. Canaan Banana

Canaan Banana alikuwa rais wa kwanza wa Zimbabwe huru Waziri Mkuu wake akiwa Robert Gabriel Mugabe.  Alikuwa mhubiri wa Kimethodisti.  Aliondolewa madarakani 1987.  Alifariki 2003

2. Praise-God Barebone

Praise-God Barebone alikuwa muuza ngozi na mhubiri wa Kiingereza.  Alichaguliwa kwenye Bunge la jamhuri ya  Uingereza mwaka 1653.  Alifariki 1679.

3. Walter Russell Brain

Baron Brain alikuwa mtaalamu wa ubongo.  Aliandika kitabu kuhusiana na magonjwa ya ubongo “Brain’s Diseases of the Nervous System”, pia akawa mhariri wa muda mrefu sana wa jarida la kitabibu liitwalo, Brain. Alipewa heshima ya kifalme mwaka 1952 akaitwa Baron Brain,1962. Alifariki 1966.

4. Marc Breedlove

Marc Breedlove ni profesa wa Neuroscience Chuo Kikuu cha Michigan State.  Anajulikana zaidi kwa utaalamu wake kuhusiana na mambo ya kujamiiana na tabia zake.

5. Thursday October Christian

Thursday October Christian mtoto wa kwanza wa Fletcher Christian (kiongozi wa uasi wa  Bounty) na mkewe Maimiti kutoka Tahiti. Alizaliwa Alhamisi ya tarehe 14 Oktoba, alipewa jina hilo kwa kuwa Fletcher Christian hakutaka kumpa mwanawe jina litakalomkumbusha Uingereza.  Thursday alifariki mwaka 1831.

6. Thomas Crapper

Crapper alikuwa fundi bomba wa Kingereza anayefahamika zaidi kwa kubuni vyoo vya kuflashi.  Alifariki mwaka 1910.

7. Prince Octopus Dzanie

Prince Octopus ni bondia wa ngumi za ridhaa kutoka Ghana aliyeshiriki Summer Olympics mwaka 2008 na michezo ya Madola 2006.

8. Argelico Fucks

Fucks ni mcheza kandanda wa Brazil.

9. Learned Hand

Learned Hand jaji wa Kimarekani na mwanafalsafa wa mambo ya sheria.  Alifariki mwaka 1961.

10. Ima Hogg

Ima Hogg, maarufu kama “The First Lady of Texas”, mmoja wa wanawake wanaoheshimika zaidi kwenye jimbo la Texas katika karne ya 20.  Alipigania sana kuondoka kigezo cha rangi na jinsia katika elimu.  Alifariki 1975.

11. Rusty Kuntz

Kuntz mchezaji wa zamani katika Ligi ya Baseball.  Sasa ni kocha wa Kansas City Royals.

12. Chuck Long

Chuck Long is the head football coach at San Diego State University. He played quarterback in college at the University of Iowa and professionally with the Detroit Lions and the Los Angeles Rams. He is an inductee of the College Football Hall of Fame.

13. Adolf Lu Hitler Marak

Adolf Lu Hitler R. Marak ni mwanasiasa wa Meghalaya, India. Jina lake si la ajabu huko Meghalaya, ambako wanasiasa wengine wamepewa majina kama Lenin R. Marak, Stalin L. Nangmin, Frankenstein W. Momin, ama Tony Curtis Lyngdoh. Hitler Marak aliliambia gazeti la Hindustan Times: “Pengine wazazi wangu walilipenda jina na wakanibatiza mimi Hitler....ninalifurahia jina langu, ingawa sina chembechembe zozote za udikteta."

14. Ten Million

Ten Million alikuwa mchezaji wa baseball na amechezea timu kadhaa katika ligi ya Northwestern katika miaka kuelekea vita ya kwanza ya dunia.  Alikuwa maarufu sana kutokana na jina lake.  Alifariki mwaka 1964

15. Chris Moneymaker

Chris Moneymaker ni mchezaji wa poka na ameshiriki katika World Series of Poker mwaka 2003.

16. Revilo Oliver

Revilo Oliver alikuwa profesa wa filolojia, Kispaniola, na Kitaliano wa Kimarekani kwenye chuo kikuu cha Illinois.  Alifariki mwaka 1994.

17. Richard Plantagenet Campbell Temple-Nugent-Brydges-Chandos-Grenville

Richard Plantagenet Campbell Temple-Nugent-Brydges-Chandos-Grenville alikuwa kiongozi wa Uingereza na rafiki wa karibu sana wa Benjamin Disraeli. Alifariki  mwaka 1889.

18. Peerless Price

Peerless Price ni wakala wa mpira wa miguu wa Kimarekani.

19. Jaime Sin

Jaime Sin alikuwa askofu wa Kifilipino bishop ambaye baadaye alikuwa Askofu Mkuu wa Kikatoliki huko Ufilipino na baadaye kuwa Kardinali Sin.  Alifariki mwaka 2005.

20. Wolfgang Wolf 

Wolfgang Wolf ni kocha wa kandanda wa Kijerumani ambaye pia amewahi kuifundisha Wolfsburg FC.

Imeandikwa na Fadhy Mtanga.


Chanzo: Listverse, tafsiri ya Kiswahili ni yangu.

Viongozi wa Kenya wanapowasaliti wananchi wao

$
0
0
JUMANNE wiki hii, macho ya Wakenya yalielekezwa mjini The Hague, Uholanzi yalipo makao ya Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya jinai (ICC).  Kizimbani anasimama makamu wa rais wa Kenya William Ruto, sambamba na mshitakiwa mwenzake Joshua arap Sang, mtangazaji wa kituo cha redio.  Wote kwa pamoja, akiwamo rais wa Kenya Uhuru Kenyatta anayetarajiwa kupanda kizimbani mwezi Novemba, wanashitakiwa kwa uhalifu dhidi ya binadamu kufuatia uchaguzi mkuu wa mwaka 2007.

Wakati hayo yakijiri, bunge la Kenya linakusudia kupitisha azimio la kutaka Kenya kujiondoa katika mkataba wa Rome ambao ndio ulioianzisha mahakama hiyo.  Wabunge wa mrengo wa Jubilee, wanataka Kenya kujiondoa kuwajibika chini ya ICC kwa minajili ya kuwanusuru viongozi wao, rais Uhuru Kenyatta, pamwe makamu wake William Ruto.  Swali la kujiuliza, viongozi wa Kenya wanawatendea haki wananchi wao?

Tujikumbushe yaliyojiri nchini Kenya takribani miaka sita nyuma.  Uchaguzi mkuu wa Kenya ulifuatiwa na vurugu kubwa.  Vurugu zilizosababishwa na matokeo ya uchaguzi ambayo watu wengi waliyalalamikia kuvurugwa.  Watu waliingia mitaani.  Kwa mapanga na silaha zingine za jadi na za kisasa.  Watu wakauawa mithili ya kuku.  Inaelezwa ni zaidi ya watu 1000 waliofariki katika sekeseke hilo.  Wanawake wakabakwa. Maelfu wakajeruhiwa. Makazi ya watu pamoja na maeneo ya biashara yakachomwa moto.  Hali hiyo ikawapelekea Wakenya takribani laki sita kukosa makazi.

Umoja wa Afrika ukaunda jopo la viongozi wanaoheshimika likiongozwa na aliyepata kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Kofi Annan.  Jopo hilo likawa na wajibu wa kuzileta pamoja pande zilizokuwa zikisigana ili kuweza kuleta amani, utulivu na maelewano miongoni mwa Wakenya.

Baada ya majadiliano ya hapa na pale hali ikarejea kawaida.  Mwezi Februari 2008, Serikali ya Kenya ikaunda tume ya kuchunguza vurugu za baada ya uchaguzi.  Tume hiyo iliongozwa na Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Philip Waki, hivyo kufahamika zaidi kama Tume ya Waki.  Tume ikafanya kazi yake ipasavyo.  Panapo Oktoba 15, 2008 tume hiyo ikakabidhi ripoti yake ya kurasa 529 kwa rais wa Kenya wa wakati huo, Mwai Kibaki.  Hata hivyo, kwa sababu za msingi kabisa, tume hiyo haikumkabidhi Mwai Kibaki orodha ya washukiwa muhimu wa sakata hilo.  Badala yake, tume ikamkabidhi majina hayo Kofi Annan aliyeongoza jopo la wasuluhishi wa mgogoro huo mbaya zaidi katika historia ya Kenya.  Mwezi Julai 2009, Kofi Annan akaikabidhi orodha hiyo kwa mwendesha mashitaka mkuu wa ICC wa wakati huo, Luis Moreno-Ocampo.

Hapo sasa, ndipo inapokuja hoja yangu kuwa viongozi wa Kenya wamewasaliti wananchi wao.  Baada ya majina kukabidhiwa ICC, Serikali ya Kenya ilipewa mwaka moja ili iunde mahakama ya ndani ya kushughulikia.  Lakini, kama kawaida ya viongozi wetu, hudhani kila upepo utapita.  Kwa bahati mbaya ya viongozi wa Kenya, upepo huu haukupita.

Kushindwa kwa Kenya kuunda mahakama kama walivyoamriwa na ICC, ndiko kulikopelekea mahakama hiyo ya kimataifa kuamua kulivalia njuga suala hilo.  Mwezi Disemba 2010, Luis Moreno-Ocampo akafanya kazi yake.  Akawasoma hadharani washukiwa hao kama ishara ya ICC kulishikia bango jambo hilo.

Hayo yamepita.  Leo hii wabunge wa Kenya wanapoamua kupitisha azimio la kuiondoa Kenya kwenye Mkataba wa Rome wanapaswa kufahamu kuwa wanawasaliti wananchi wao ambao waliathiriwa kwa kiasi kikubwa na vurugu zile zilizochochewa na wanasiasa na wafanyabiashara kwa maslahi yao binafsi.  Lakini pia, wanapaswa kukumbuka kuwa walipewa muda wa kutosha ili waweze kuunda mahakama ya ndani ya kushughulikia jambo hilo.  Kwa sababu wanazozifahamu wao wenyewe, mahakama hiyo haikuundwa.  Kutoundwa kwa mahakama hiyo ndiko kulikopelekea viongozi wa Kenya kulazimika kusafiri hadi The Hague, ili kukabiliana na mahakama hiyo ya juu zaidi.

Viongozi wa mrengo wa Jubilee pengine hawajapata ushauri wa kisheria wa kutosha.  Wakati wao wanakusudia kumwokoa rais wao, wanatakiwa kukumbuka kuwa kwa mujibu wa mkataba huo, endapo nchi mwanachama itaamua kujiondoa, kujiondoa huko hakutoathiri kesi ambazo tayari zinaendelea.  Kwa mantiki hiyo, hatua hiyo ya Kenya itayahusu tu mambo ambayo yatatokea baada ya Kenya kuwa imejiondoa.  Azimio la Kenya kujiondoa linatakiwa kuwasilishwa katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa likiwa na sababu za kutosha za kwa nini Kenya inakusudia kujitenga.  Idhini ya Kenya kujitenga inachukuwa takribani mwaka mzima ili iweze kutolewa.

Viongozi wa Kenya, hata kama watapitisha azimio lao, wanapaswa kujikumbusha  kuwa hawatofanikiwa kuwaokoa Uhuru Kenyatta na William Ruto.  Washitakiwa hawa wataendelea kukabiliana na mashitaka dhidi yao.  Lakini pia, hata kama nchi siyo mwanachama wa ICC, haiwapi kinga watu wake kutoshitakiwa na mahakama hiyo.  Watazame mfano wa Sudan ambayo siyo mwanachama.  Rais wake Omar al-Bashir ana kesi katika mahakama hiyo.  Waranti ya kukamatwa kwake ilishatolewa.  Leo anaishi kwa mashaka akiogopa kusafiri kwenda baadhi ya nchi akihofia kukamatwa.

Hivyo, Kenya ikijitoa haitoweza kuzuia viongozi wake kukamatwa.  ICC haina polisi.  Kwa mujibu wa mkataba wa Rome, mahakama hiyo hutegemea polisi wa nchi wanachama.  Nchi wanachama zinawajibika kutoa ushirikiano katika kuwakamata watuhumiwa wa mahakama hiyo.  Viongozi wa Kenya hawalijui hili?

Kuiondoa Kenya kutoka Mkataba wa Rome ni kuwasaliti wananchi wake.  Ni kutaka kuwaambia kuwa wao hawatoogopa kuendesha vurugu zozote za uchaguzi na nyinginezo kwa kuwa hawatokuwa wakiihofia mahakama ya kimataifa.  Kama walivyojinadi wakati wa uchaguzi uliomwingiza Uhuru Kenyatta madarakani, hawababaishwi na mashinikizo ya mataifa ya magharibi.  Wakati wakijinadi hivyo, wanapaswa kukumbuka uhai na ustawi wa wananchi wao ni muhimu kuzingatiwa kuliko kile wanachokiita kelele za mataifa ya magharibi.

Nimalizie kwa kuwakumbusha viongozi wa Kenya.  Wao wenyewe ndiyo waliolipuuza agizo la ICC la kuunda mahakama ya ndani kushughulikia mambo hayo.  Viongozi wao walipelekwa ICC kwa kuwa wao ndani walishindwa kuandaa mchakato wa kuhakikisha haki inatendeka.  Kwa mantiki hiyo, kwa sasa hawana pa kutokea, wala hawana sababu za msingi za kuieleza jamii.  Isipokuwa, kwa sababu tu za kulindana huku wakiwasaliti wananchi wao ambao ndiyo wahanga wakubwa.


Ukiudharau mwiba, mguu huota tende.

Kwa nini nchi za Afrika zinaihara ICC?

$
0
0
MASHIRIKA ya habari yana ripoti juu ya kile kinachoendelea jijini Adis Ababa, Ethiopia kunakofanyika mkutano wa Umoja wa Afrika (AU).  Wakati mkutano huo ukiendelea, Kenya na Sudan zinasemekana kuwa katika mstari wa mbele kuzishawishi nchi zingine za Kiafrika kuisusia Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC).

Hatua hiyo inafuatia kesi kabambe iliyopo ICC ambapo rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta pamwe makamu wake William Ruto wanatuhumiwa kwa kusababisha vurug za uchaguzi wa Kenya mwaka 2007.  Kumekuwa na jitihada za makusudi kutoka ndani ya Kenya, hususani kwa wabunge wa Jubilee wakitaka Kenya kujiondoa kwenye Mkataba wa Roma ulioanzisha mahakama hiyo.

Jitihada hizo zimetua rasmi jijini Adis Ababa ambapo chombo kikubwa zaidi barani Afrika kinaketi.  Sote tunafahamu kwa nini ni Kenya na Sudan walio mstari wa mbele kushawishi nchi 34 za Kiafrika zilizotia saini Mkataba wa Roma kuisusia ICC.  Wakati rais wa Kenya na makamu wake wakiwa na kesi, naye rais wa Sudan, Omar al-Bashir alishatolewa hati ya kukamatwa kwake.  Ndiyo sababu iliyoifanya hata Marekani kumnyima viza ya kuingia nchini humo kuhudhuria mkutano wa Umoja wa Mataifa majuma machache yaliyopita.

Balozi wa Sudan huko Adis Ababa, bwana Abdul-Rahman Siralkhatim amenukuliwa jana akidai kuwa kitendo hicho cha viongozi wa Kiafrika kinatarajiwa kuwa cha kihistoria zaidi dhidi ya ukandamizaji unaofanywa na mataifa ya Magharibi kwa nchi za Kiafrika.

Kwa nini nchi za Kiafrika haziitaki ICC?  Ni kwa sababu ya ukandamizaji wa Kimagharibi dhidi ya nchi zetu za Kiafrika?  Kwa mtazamo wangu, sababu ni zaidi ya hiyo.  Kama tatizo ni ukandamizaji wa mataifa ya Kimagharibi, hapana shaka nchi za Kiafrika zingekuwa mstari wa mbele kusimama imara kwa pamoja kupinga ukandamizaji wa kiuchumi unaofanya na wawekezaji wa mataifa ya Ulaya na Asia.

Hizi nchi zinazosema mataifa ya Magharibi yanatukandamiza Waafrika kwa kupitia ICC ndizo zilizo mstari wa kwanza kutoa misamaha mikubwa ya kodi kwa makampuni makubwa ya Magharibi yanayokuja kwa mwamvuli wa uwekezaji huku yakikwangua pasi huruma rasilimali zote za Afrika.  Busara kubwa kwa nchi za Afrika, bara lenye wakazi zaidi ya bilioni moja ikiwa ni zaidi ya asilimia 15 ya idadi ya watu ulimwenguni, ingekuwa ni kwa nchi hizi kuikata mirija ya unyonyaji kutoka kwa mataifa tajiri duniani.  Hili lingewezekana kwa nchi za Kiafrika kuungana pamoja katika kuzisimamia vema rasilimali zilizopo.  Kama nchi ya China imefanikiwa ikijivunia idadi yake ya watu, nchi za Afrika zinashindwa nini?

Leo hii, nchi za Kiafrika zinaiona ICC kama adui yao mkubwa kwa kuwa tu imewagusa wakubwa wenzao.  Lakini tujiulize swali la msingi.  Si kweli ukatili dhidi ya binadamu ulitokea Kenya ama Sudan?  ICC inaweza ikawa na matatizo yake ya kimfumo na utendaji wa kazi.  Tunarejea kwenye busara ya kisheria, makosa mawili hayalihalalishi kosa la pili.

Nchi za Kiafrika zinatambua vema juu ya Wakenya zaidi ya 1000 waliopoteza maisha kufuatia vurugu zile.  Zinafahamu vema juu ya wengine zaidi ya laki sita waliopoteza makazi yao.  Si hilo tu, zinafahamu vema juu ya ripoti ya kurasa 529 ya Tume ya Waki iliyoundwa kuchunguza kiini na wasababishi wa kadhia ile mbaya kabisa katika historia ya taifa hilo la Afrika Mashariki.  Bila shaka pia, nchi hizi za Kiafrika zinakumbuka vema namna mwendesha mashtaka wa ICC wa wakati huo Luis Moreno-Ocampo alivyozipa mamlaka za Kenya mwaka mmoja ili ziweze kuunda chombo cha ndani cha kuwahukumu watuhumiwa hao.  Kenya ikapuuza kufanya hivyo.

Leo hii, jijini Adis Ababa, viongozi wetu wanatuambia mambo ya Afrika yatasimamiwa na Waafrika wenyewe.  Tunajifunza nini kwa mfano huu wa Kenya ilipopewa mwaka mmoja wa kuunda mahakama ya ndani nayo ikapuuza kufanya hivyo?  Tunawaza nini kujisahaulisha kuwa hatua ya ICC kuwafungulia kesi Uhuru na wenzake ilitokana nasi Waafrika wenyewe kupuuza agizo la kujihukumu wenyewe?

Endapo nchi za Afrika zitajitoa kwenye Mkataba wa Roma na hivyo kuamua kutoipa ushirikiano ICC, litakuwa pigo kubwa mno kwa Waafrika.  Hatua hiyo itafungua milango kwa ukandamizaji dhidi ya haki za kibinadamu.  Itafungua milango kwa matukio mengi ya ukatili dhidi ya binadamu huku viongozi wa Afrika wakijivunia kutowajibika pahala popote katika ngazi ya kimataifa.

Wasiwasi wangu ungalipo.  Kiongozi anapoukataa mfumo wa kisheria unaomsimamia namna afanyavyo kazi zake, hapana shaka anataka kuwa juu ya sheria.  Madhara ya kuwa na viongozi walio juu ya sheria ni makubwa mno kwa watawaliwa ambao kwa kawaida ni watu wa chini wasio na nguvu yoyote nje ya sheria kuuondoa ukandamizaji wowote dhidi yao.

Hatua hii ya viongozi wa Afrika inapaswa kutazamwa kwa jicho la usaliti dhidi ya Waafrika wenzao.  Inapaswa kueleweka kama hatua inayokusudia kupiga mhuri wa moto kwenye mamlaka zisizo na kikomo kwa viongozi wa Afrika.

Kama sivyo, kwa nini nchi za Afrika zinaihara ICC?

Fadhy Mtanga,
Dar es Salaam.
Ijumaa, Oktoba 11, 2013.

Riwaya ya Huba

$
0
0

HABARI za siku tele?
Ni muda mrefu umepita sijaandika humu. Ukimya wangu haukuwa bure.  Nilikuwa jikoni nikiandaa pishi.
Sasa pishi limeiva.  Ni riwaya ya HUBA.  Kama lilivyo jina la kitabu, ni simulizi yenye mkasa wa mapenzi. Yumo Zedi. Yumo July. Yumo Rose. Hawa wanashiriki kizungumkuti cha Huba.
Wamo Jerry na Shania. Marafiki wa kweli daima.
Ni Huba.
Kitakuwa tayari panapo Mei 10, 2014.
Usikose nakala yako kwa kuwasiliana nami katika 0715 599 646 ama fadhymtanga@gmail.com

Nimerejea rasmi kublog

$
0
0



Ni muda mrefu sana umepita tangu nilipoweka bandiko kwa mara ya mwisho hapa kibarazani kwangu.  Marafiki zangu wamekuwa wakiniuliza mara kwa mara juu ya kupotea kwangu katika kublog.

Sikuwa na sababu ya msingi kuacha kuweka mabandiko.  Ni kapepo tu ka-uvivu kalikoniandama.

Nimekakemea kwa nguvu zote.

Ninasikia furaha kusema, nimerejea kublog.  Panapo majaaliwa, kwa picha na makala kadha wa kadha, kwa mtazamo wangu, Mwananchi Mimi.

Tuzidi kuwa pamoja.

Fadhy,
Mbeya, Tanzania.
Jumatano, Disemba 2, 2015.

Kakao kutoka Matema

$
0
0


Tunda la kakao, kijijini Kisyosyo, kata ya Matema, wilayani Kyela, mkoani Mbeya,

Ni utajiri unaowazunguka wananchi.  Lakini, ni wazi hauwanufaishi kwa kiwango cha kuridhisha.

Mapambazuko ziwani Nyasa

$
0
0


Asubuhi ya leo hapa ufukwe wa Matema, Kyela mkoani Mbeya..  Nikiitazama nuru ya jua ikichomoza kwa mbali, mashariki, nyuma ya milima ya Livingstone.

Barabara ya Matema

$
0
0

Barabara iendayo ufukwe wa Matema.  Niliipiga picha hii jana mchana.

Kwa miaka mingi, barabara hii haikupewa kipaumbele ili ijengwe katika kiwango cha lami.  Angalau sasa, ujenzi wa barabara hii katika kiwango cha lami u mbioni kuanza.

Hili ni eneo ambalo, kama barabara ya lami ikijengwa, itasaidia sana kuinua uchumi wa wakazi wa maeneo ya Matema, Ipindi, Tenende na maeneo mengine ya jirani, hatimaye wilaya ya Kyela kiujumla.

Eneo hili ni maarufu sana kwa kilimo cha mpunga (ule mchele maarufu sana wa Kyela), kakao, michikichi na matunda ya aina mbalimbali.  Si hivyo tu, sekta ya utalii itakuwa kwa kuwa sasa watu wengi watamudu kusafiri kwa urahisi ili kuufikia ufukwe maarufu katika Ziwa Nyasa, Matema.

Si hivyo tu, upandaji wa safu za milima ya Livingstone ni moja ya vivutio muhimu katika sekta ya utalii.

Vijana wengi ndani ya maeneo haya, wanayo matumaini makubwa sana juu ya uwepo wa barabara ya lami.  Wanaamini itawarahisishia kufikia masoko ya bidhaa zao, hivyo kubadili maisha yako.



Gari majini

$
0
0

Wanasema, tembea uone.

Nami nimeona.

Maisha ziwani

$
0
0


Maandalizi kwa ajili ya uvuvi usiku wa leo.  Mchana huu hapa ufukweni Matema, Ziwa Nyasa.

Mambo Niliyojifunza Mwaka 2015

$
0
0


Wakati mwaka ndiyo umefika ukingoni, ninaketi chini.  Ninatafakari.  Ninajikuta ninazikumbuka vema siku 365 za mwaka 2015.  Kila siku moja, ilikuwa ni ukurasa moja katika kitabu cha 2015.  Kila ukurasa, umenifunza mambo mengi sana.  Ninayaazima maneno ya Mwanamapinduzi na Sauti ya Ghetto, Bob Marley, “What life has taught me, I would like to share; with those, who want to learn.”

Hivyo, yale niliyojifunza, ningependa kuwashirikisha; wale, watakao kujifunza.

1. Kuishi kwa malengo ni muhimu sana.  Ukiishi kwa malengo utafahamu wakati wa kusema ndiyo, na wakati wa kusema hapana.

2. Ni vema kuwajali wazazi.  Wapo wengi wanaotamani kuwa na wazazi lakini hawana.  Hivyo, kama umebahatika kuwa nao, wathamini kwa kuwa hawana mbadala.

3. Ni muhimu kuijali afya.  Katika yote uyafanyayo, jitahidi kuilinda afya yako.

4. Hakuna wakati sahihi utakaokuwa tayari.  Ukitaka kufanya jambo, usiseme unasubiri wakati utakaokuwa tayari.  Wakati huo hautofika kamwe.  Wakati ni uliopo.  Anzia pale pale ulipo.


5. Kuna tofauti kubwa sana kati ya kukata tamaa na kuacha kupoteza muda. Unaweza ukajua wewe si mtu wa kukata tamaa, kumbe ni mpoteza muda. Jifunze kutofautisha vema kutokana na muktadha wa jambo husika.

6. Hatuzaliwi na hamasa fulani. Tunajifunza kadri tunavyojizowesha kuyatazama mambo yanayotuzunguka kwa macho chanya.  Ukiweza kulitazama kila jambo kwa macho chanya, kila jambo litakuwa jema kwako.

7. Mahusiano ni jambo muhimu sana.  Mahusiano yenye afya huchochea ufanisi katika mambo mengi.  Na kinyume chake.

8. Kuna kitu kimoja tu duniani kinachoweza kubadili nafasi ya furaha. Kitu hicho ni, furaha.  Lakini kama ni pesa ndizo zikupazo furaha,  furaha yako ingali na walakini. Ingawa, wanasema, kuna tofauti kubwa unapolia ndani ya daladala, na unapolia ndani ya Range Rover.

9. Lakini, kama furaha yako inasababishwa na mtu mwingine, bado hujaipata.  Furaha yako inatakiwa iwe juu ya viganja vyako.  Huku ukifahamu kuwa, ukivibinua, basi umeimwaga.  Japo, mtu mwingine hapaswi kuwa chanzo cha furaha yako, kamwe, usiwe chanzo cha mtu mwingine kukosa furaha.

10. Maua mengi yavutiayo duniani, huchanua kutoka katika mashina yasiyovutia machoni, mengine, yakiwa yamesheheni miba. Yatazame maisha yako kwa mfano wa maua.  Usiumizwe na mashina ya maisha.  Furahia kichanuacho juu ya mashina hayo.

11. Kusikiliza muziki uupendao kila siku kunakufanya uzidi kuyafurahia maisha. Ukijenga mazowea ya kusikiliza muziki uupendao kila siku, wakati mwingine kuuigiza kuuimba, maisha yako yatajaa furaha.

12.  Kamwe, mafanikio hayatokuletea furaha.  Bali, furaha yako ndicho chanzo kikuu cha mafanikio yako.

13. Furahia wakati uliopo.  Usisubiri kusema ya kale dhahabu.  Tambua, ya sasa ni almasi.

14. Ni muhimu sana kufanya makosa katika maisha.  Kamwe, usiogope kufanya makosa katika maisha yako.  Usiogope kumkosea mpenzi wako, mzazi wako, rafiki yako, mkubwa wako, mdogo wako, jirani yako, ama yeyote yule.  Fanya makosa mengi kadri uwezavyo.  Makosa ndiyo ukamilifu wa ubinadamu wako.  Lakini, ni mwerevu tu, ayatazamaye makosa kwa macho chanya.  Makosa, ndiyo yatufanyayo kuwa imara.

15. Kuandika na kusoma mara kwa mara kunaongeza uwezo wa kufikiri.  Kunaliwaza moyo.  Kunachochea furaha ndani yako.

16. Ukiona uvivu kupika, mtu anaweza kukupikia. Ukiona uvivu kufua, mtu anaweza kukufulia. Lakini, ukiona uvivu kuandika, hakuna wa kukuandikia.  Unapoona uvivu kuziandika fikra zako ili zisomwe na wengine, kumbuka haya.

17. Unaweza kutingwa kukusanya mawe huku huioni almasi miguuni pako.  Tazama kwa macho chanya, maangavu yale yakuzungukayo.

18. Kama unataka kufeli maishani mwako, basi jaribu kumridhisha kila mtu.

19. Mara zote, watu tunaoepuka sana kuwaumiza maishani, ni wale wasiojali kutuumiza.

20. Usimlaumu mtu mwingine kwa jambo lolote maishani mwako. Jitafakari.

21. Kusafiri sana na kukutana na watu tofauti tofauti kunakufanya ujifunze mambo mengi sana na kuyafurahia maisha.

22. Jifunze kumshukuru Mungu kwa kila jambo.

23. Ingawa wanasema heri huzaliwa katika tumbo la shari, likuepukalo lina heri nawe.

Zaidi ya yote, ni vema kuishi maisha ya kumtegemea na kumwadubu Mungu pekee.


Wanasema, kuishi ni kujifunza.  Nami, naufurahi sana uanafunzi wangu.

Mwaka ndo ushaisha. Kama hukuuanika, bila shaka umeutwanga mbichi.  Nakutakia heri katika kuumaliza mwaka 2015 na kuukaribisha Mwaka Mpya wa 2016.  Mwenyezi Mungu azidi kukubariki.

Fadhy Mtanga,
Mbeya, Tanzania.
Alhamisi, Disemba 31, 2015.

Safu za Milima ya Livingstone

$
0
0

Kama ionekanavyo kutoka mjini Kyela. Katika siku ya Mwaka Mpya wa 2016.

Matunda hayakauki Mbeya

$
0
0

Kila msimu na matunda yake.

Kijijini Isyonje, wilaya ya Rungwe, Mbeya. Leo alasiri.

Viewing all 76 articles
Browse latest View live