Heri ya siku ya kuzaliwa mama yangu mpenzi. Leo tarehe 18 Januari ni siku muhimu sana kwangu. Ni siku ambayo mama yangu mpenzi ulikuja duniani. Ni siku iliyoandaa uwepo wangu duniani.
Mama, leo tunapoikumbuka siku hii ya thamani zaidi, napenda kukwambiia kuwa ninakupenda sana. Kwangu hakuna zaidi yako. Ninamshukuru sana Mungu kwa ajili yako. Ninamshukuru sana Mungu kwa kuwa pamoja na kunilea kwako ukiwa peke yako, umenifanya kuwa hivi nilivyo leo. Ninajivunia sana wewe.
Ninakushukuru sana mama kwani magumu yangu yamekuwa yako pia, mepesi yangu yamekuwa yako pia. Umekuwa ukiniunga mkono daima. Umekuwa ukinikosoa pale nipotokapo. Umekuwa ukinifuta machozi na kunikumbatia hata wengine wote wanipapo kisogo. Umekuwa ukinipa moyo wengine wanineneapo ubaya. Kwangu, wewe ni mwanamke wa shoka.
Mama, leo ni siku muhimu sana kwangu. Ninakuombea maisha marefu sana, yenye furaha tele, afya njema, na mafanikio zaidi. Ninakupenda sana mama yangu. Ninakupenda mno. Ninamshukuru sana Mungu kwa kunipa wewe kama mama yangu.
HAPPY BIRTHDAY MY LOVELY MOM!
Mama, leo tunapoikumbuka siku hii ya thamani zaidi, napenda kukwambiia kuwa ninakupenda sana. Kwangu hakuna zaidi yako. Ninamshukuru sana Mungu kwa ajili yako. Ninamshukuru sana Mungu kwa kuwa pamoja na kunilea kwako ukiwa peke yako, umenifanya kuwa hivi nilivyo leo. Ninajivunia sana wewe.
Ninakushukuru sana mama kwani magumu yangu yamekuwa yako pia, mepesi yangu yamekuwa yako pia. Umekuwa ukiniunga mkono daima. Umekuwa ukinikosoa pale nipotokapo. Umekuwa ukinifuta machozi na kunikumbatia hata wengine wote wanipapo kisogo. Umekuwa ukinipa moyo wengine wanineneapo ubaya. Kwangu, wewe ni mwanamke wa shoka.
Mama, leo ni siku muhimu sana kwangu. Ninakuombea maisha marefu sana, yenye furaha tele, afya njema, na mafanikio zaidi. Ninakupenda sana mama yangu. Ninakupenda mno. Ninamshukuru sana Mungu kwa kunipa wewe kama mama yangu.
HAPPY BIRTHDAY MY LOVELY MOM!